KIDATO CHA NNE 2022

   102/3- KISWAHILI – Karatasi   ya Tatu

FASIHI- 2022- Muda:  – Saa 2

1.SEHEMU YA ‘A’:  USHAIRI (LAZIMA)

Eti

Mimi niondoke hapa

Niondoke hapa kwangu

Nimesaki, licha ya risasi

Vitisho na mauaji, siondoki

Mimi

Siondoki

Siondoki siondoki

Niondoke hapa kwangu!

Kwa mateke hata na mikuki

Marungu na bunduki, siondoki

Hapa

Siondoki

Mimi ni Pahame!

Niondoke hapa kwangu!

Fujo na ghasia zikizuka

Na kani ya waporaji, siondoki

Haki

Siondoki

Kwangu siondoki

Niondoke hapa kwangu!

Nawaje; waje wanaokuja

Mabepari wadhalimu, siondoki

Kamwe

Siondoki

Ng’oo hapa kwangu!

Katizame chini mti ule!

Walizikwa babu zangu, siondoki

Sendi

Nende wapi?

Si hapa kitovu changu

Niondoke hapa kwangu

Wangawa na vijikaratasi

Si kwamba hapa si kwangu, siondoki

Katu

Siondoki

Sihitaji karatasi

Niondoke hapa kwangu

Yangu mimi ni ardhi hii

Wala si makaratasi, siondoki

Maswali

a)         Shairi hili ni la aina gani? Kwa nini?                           (alama 2)

b)         Taja masaibu anayopitia mzungumzaji.                                   (alama 4)

c)         Eleza toni ya shairi hili.                                                           (alama 2)

d)         Eleza muundo wa shairi hili.                                       (alama 3)

e)         Tambua matumizi ya mbinu ya usambamba.              (alama 2)

f)         Andika ubeti wa tano kwa lugha nathari        .                       (alama 4)

g)         Tambua idhini moja ya mtunzi.                                               (alama 1)

h)         Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika shairi.  (alama 3)

            (i) karatasi

            (ii) nimesaki    

            (iii) kitovu

            SEHEMU YA B:TAMTHILIA: Kigogo, P. Kea

2. “Na hiyo sauti ya Jabali imekuwa adha. Inanikama roho….”

  • Eleza muktadha wa dondoo hili.                                                                       (alama 4)                                                                             
  • Tambua mbinu mbili za lugha zilizotumika dondooni.                                     (alama 2)                        
  • Kwa hoja kumi na nne fafanua matendo yanayomkaba roho msemaji.       (alama 14)

3. Eleza athari kumi za tamaa na ubinafsi kwakurejelea tamthilia ya Kigogo.     (alama20)

SEHEMU YA C:RIWAYA: Chozi la Heri, A. Matei          

   4. “Sisi tunataka kiongozi yeyote, awe mwanamke au mwanamume, atakayewezakulielekeza jahazi hili letu kwenye visiwa vyahazina.”

a) Eleza muktadha wadondoo hili.                                                                     (alama 4)

b) Bainisha mbinu nne za lugha zinazojitokeza katikadondoo hili.                       (alama 4)

c) Huku ukirejelea riwaya Chozi la Heri, jadili mchango wa warejelewa katikakuboresha maisha ya Wahafidhina kwa hoja kuminambili.               (alama 12)

5. a) “Na kuwe huko kumtoa mekoni lakini hili la kumpa jukumu la kuliongoza jamii nzima! Itakuwa kukivika kichwa cha kukukilemba.”

                (i) Bainisha toni inayojitokeza katikadondoohili.                                          (alama 2)

               (ii) Linganisha na ulinganue msemaji na msemewa katikadondoohili.          (alama 9)      

b)Changanuamtindo katika dondoo hili.                                                         (alama 9)

“Kumbe wewe ni sawa na yule Mwangeka wa kihistoria ambaye kivuli chake kikitembea siku zote mbele yake, ambaye mwili wake ulikuwa kaka tu,roho yenyewe iliishinje ya kaka hili kwa kutotaka kuthibitiwa? Umewezaje kunusurika? Kumbe huo wadhifa waliokupa wa kwenda kudumisha amani Mashariki ya Kati umetokea kuwa wongofu wako? Maskini Lily mkaza mwanangu! Umekuwa kama jani linalopukutika msimu wa machipuko! Umetoweka katika ulimwengu huu ukiwa teketeke, hata ubwabwa wa shingo haujakutoka!”

SEHEMU YA D: Hadithi Fupi

 A. Chokocho na D. Kayanda(Wahariri), Tumbona Hadithi na NyingineLisiloshiba

Jibu swali la 6 au 7

6.Ukirejelea hadithi zifuatazo, eleza jinsi maudhui ya mapenzi na asasi ya ndoa yanavyojitokeza.                                                                                      (alama20)

a)Mapenzi ya Kifaurongo

b)Masharti ya Kisasa

c)Ndoto ya Mashaka

d)Mtihani wa Maisha

7.         Salma Omar Hamad,Shibe Inatumaliza

a) “Wanafanya kazi ya ukwe tu. Hawana wasichofanya lakini hawanawafanyacho.

  i) Bainisha tamathali tatu za usemi zinazojitokeza katikadondoohili. (alama 3)

ii) Kwa hoja zozote nane, thibitisha ukweli wa kauli iliyokolezwa huku ukirejeleahadithi Shibe Inatumaliza.(alama8)

Alifa Chokocho,Tulipokutana tena

b)‘Pale nilipokwenda kulelewa palikuwa jahanamukwangu.”

Tathmini ukweli wa maneno haya ukirejelea hadithi ‘Tulipokutana Tena’.                 (alama 9)

SEHEMU YA E: FASIHI SIMULIZI

  • a) Eleza maana ya vipera vifuatavyo vya fasihi simulizi.                                      (alama 8)

            (i)misimu

                       (ii)ngomezi

          (iii)miviga

          (iv)maapizo      

b) (i) Fafanua dhima sita za miviga katika jamii yako.                                           (alama 6)       (ii) Tambulisha sifa zozote sita za misimu.                                                              (alama 6)

Huu ndio ukurasa wa mwisho uliopigwa chapa maswali.

………………………………………………………………………………………………………

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *